Hiki ndiyo chakula kocha Moyes aliwanyima wachezaji wa Manchester united kula
TZ MZUKA
09:03
0
Miezi takribani 10 tangu atimuliwe kutoka kwenye nafasi ya ukocha wa klabu yaManchester United, David Moyes ameelezea moja ya jambo lilokuwa linaisibu timu ya Manchester United wakati wa utawala wake na kutishia mafanikio ya timu uwanjani.
Akihojiwa na jarida maarufu la soka la FourFourTwo, David Moyes ambaye kwa sasa anaifundisha timu ya Real Sociedad ya Uhispania alisema tatizo kubwa lilokuwa linaisumbua timu lilikuwa ni wachezaji wengi kuwa na uzito uliopitiliza (Ubonge), kitu kilichopelekea aamue kuwapiga marufuku kabisa matumizi ya chips kwa wachezaji wake.
“Ndio, ilibidi nipige marufuku chips“– Moyes.
“Ilikuwa kwa sababu kulikuwa na wachezaji wengi ambao walikuwa na uzito uliopitiliza na sikudhani kama chips zilikuwa nzuri kwenye diet yao, hivyo nikapiga marufuku.”– Moyes