UEFA CHAMPIONS LEAGUE: BARCELONA 1 vs 0 MANCHESTER CITY IVAN RAKITIC AIPA USHINDI BARCA, SERGIO AGUERO AKOSA PENATI!! MAN CITY NJE UEFA!!
TZ MZUKA
14:58
0
Barcelona imefanikiwa kufuzu Robo Fainali ya Kombe laMabingwa Ulaya baada ya leo kuifunga Manchester City bao 1-0 lililofungwa na Ivan Rakitic dakika ya 31 na kuitupa nje kwa jumla ya mabao 3-1 baada ya ushindi wa 2-1 ilioupata katika mchezowa kwanza.
Katika mchezo wa leo Sergio Aguero amepoteza nafasi ya kuipatia Man City bao baada ya kupoteza mkwaju wa penati katika Dakika ya 78 baada ya mkwaju wake kuokolewa na kipa wa Barcelona.
Katika mchezo mwingine Juventus imeifunga Borussia Dortmund mabao 3-0 katika mchezo uliopigwa nchini Ujerumani, na kufanya Juventus ifuzu Robo Fainali kwa jumla ya mabao 5-1 baaada ya kushinda 2-1 katika mchezo wa kwanza.
Mechi za leo zimehitimisha jumla ya timu 8 zilizofuzu Robo Fainali ambazo ni Barcelona, Juventus, Monaco, Atletico Madrid, Real Madrid, Bayern Munich, PSG na FC Porto.

Barcelona: Ter Stegen, Dani Alves, Pique, Mathieu, Jordi Alba, Rakitic, Mascherano, Iniesta, Messi, Suarez, Neymar.
Akiba: Bravo, Xavi, Pedro, Rafinha, Bartra, Sergi Roberto, Adriano.
Manchester City: Hart, Sagna, Kompany, Demichelis, Kolarov, Nasri, Toure, Fernandinho, Milner, Silva, Aguero.
Akiba: Caballero, Zabaleta, Fernando, Dzeko, Bony, Jesus Navas, Lampard.
Refa: Gianluca Rocchi

