Select Menu
Select Menu

Sports

Sports

Entertainment

Music

Video

News

Video

» » Bei Ya Tiketi Za Kushuhudia Pambano La Mayweather Vs Pacquiao.


TZ MZUKA 11:28 0

Zikiwa zimebaki siku 9 kabla ya pambano lilopewa jina la ‘Fight of the Century’ kati ya mwanasumbwi tajiri zaidi duniani ‘Floyd Mayweathe Jr’ ambaye ana rekodi ya kutopoteza pambano hata moja tangu aanze kucheza mchezo huo, dhidi ya mfilipino mwenye rekodi nzuri kabisa Manny Pacquiao kufanyika, leo hii bei ya viingilio vya kutazama mchezo huo imetangazwa.

Unaambiwa tiketi ya bei ya chini kabisa itakayokuwezesha kuingia MGM Grand Garden Arena itakuwa ikiuzwa kwa $1500 ambayo ni zaidi ya millioni 2.5 ya Kitanzania.

Kwa wale vibopa ambao wa kati tiketi zao zitauzwa kwa $7500. 
Tiketi hizi zitaanza kuuzwa leo usiku saa 2 kwa saa za Marekani, na kundi hili za tiketi litahusisha uuzwaji wa tiketi 1000 tu.

Wakati huo huo zimetengwa tiketi za bei ya juu zaidi ambazo zitakuwa kwa $10,000 huku nyingine zikiuzwa kwa $200,000 kwa watu mashuhuri wenye uwezo wao.

Pia kwa wale watakaoshindwa kulipa viingilio hivyo, umeandaliwa mpango kuandaa sehemu itakayoingiza watu 50,000 ambao watalipa viingilio $150.

«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani