Select Menu
Select Menu

Sports

Sports

Entertainment

Music

Video

News

Video

» » Mke wa Shetta alikataa gari alilonunuliwa na mumewe


TZ MZUKA 09:18 0

Ndoa ya Shetta bado ipo kwenye mawe! Muimbaji huyo wa ‘Shikorobo’ na mke wake Mama Qayllah bado hawana maelewano mazuri kiasi ambacho amelikataa gari alilonunuliwa na mumewe hivi karibuni.

Shetta amekiambia kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM kuwa Mama Qayllah amekataa kurejea nyumbani licha ya kumletea zawadi ya gari ambayo alimuahidi kipindi cha nyuma.
“Yeah nimemnunulia gari mpya lakini amelikataa,” alisema Shettah. “Hili gari nilimuahidi nimtamnunulia toka zamani na lilikuwa njiani sasa limeingia na nimelichukua wakati yeye hayupo nyumbani. Nimemwambia gari lake lipo tayari lakini amekataa. Mama Qayllah hayupo nyumbani, mimi kama ananisikiliza naomba arudi nyumbani.”

«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani