Select Menu
Select Menu

Sports

Sports

Entertainment

Music

Video

News

Video

» » UEFA CHAMPIONS :Matokeo ya Schalke na Real Madrid CF Ronaldo aibeba Real


TZ MZUKA 14:24 0

 
MCHEZAJI BORA Duniani Cristiano Ronaldo, ameiongoza Timu yake Real Madrid kuifunga Schalke Bao 2-0 huko Gelsenkirchen katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Hadi Mapumziko Real walikuwa mbele kwa Bao la Cristiano Ronaldo la Dakika ya 26 ambalo limemaliza ukame wake wa kutofunga katika Mechi 3 zilizopita za Real.
Bao hilo lilitokana na Krosi ya Fulbeki Carvajal aliyomimina kutoka Kulia na Ronaldo kuunganisha kwa Kichwa na kumzidi maarifa Kipa Wellenreuther.
Real walipiga Bao lao la Pili Dakika ya 79 kufuatia Ronaldo, akiwa Winga ya Kushoto, kuwatambuka Mabeki wawili na kumlisha Marcelo alietumbukia ndani ya Boksi na kuachia kigongo kwa Mguu wake ‘dhaifu’ wa Kulia na kutingisha nyavu.
Marudiano ya Timu hizi ni huko Santiago Bernabeu Jijini Madrid hapo Jumanne Machi 10 na Mshindi kutinga Robo Fainali.
VIKOSI:
SCHALKE: Wellenreuther; Uchida, Howedes, Matip, Nastasic, Aogo; Hoger (Meyer - 80'), Neustadter (Kirchhoff - 57'), Boateng; Choupo-Moting, Huntelaar (Platte - 33')
Akiba: Wetklo, Kirchhoff, Meyer, Fuchs, Ayhan, Barnetta, Platte.
REAL MADRID: Casillas; Carvajal (Arbeloa - 82'), Varane, Pepe, Marcelo; Lucas Silva, Kroos, Isco (Illarramendi - 85'); Bale, Benzema (Hernández - 78'), Ronaldo
Akiba: Navas, Hernandez, Arbeloa, Nacho, Jese, Illarramendi, Medran.
MATOKEO MENGINE

FC BASEL 1 FC PORTO 1
FC Basel na FC porto zimetoka Sare ya Bao 1-1 huko Uswisi katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Mpaka Mapumziko FC Basel walikuwa mbele kwa Bao la Derlis Gonzalez la Dakika ya 11.
Porto walisawazisha Dakika ya 48 kupitia Casemiro, Mchezaji wa Mkopo kutoka Real Madrid, lakini Refa Mwingereza Mark Clattenburg alibadili uamuzi wake baada ya Msaidizi wake kuashiria ni Ofsaidi.
Hata hivyo, Porto walisawazisha kwa Penati ya utata ya Dakika ya 79 iliyofungwa na Danilo Luiz da Silva.
Penati hiyo ilitolewa kufuatia Refa Clattenburg kuamua Clattenburg Walter Samuel kaunawa Mpira.
Marudiano ya Timu hizi ni huko Ureno hapo Jumanne Machi 10 na Mshindi kutinga Robo Fainali.
VIKOSI:
FC BASEL: Vaclik, Xhaka, Suchy, Samuel, Safari, Gonzalez (Callà - 25'), El-Nenny, Frei, Zuffi, Gashi Hamoudi - 83'), Streller (Embolo - 63')
Akiba: Vailati, Degen, Arlind Ajeti, Delgado, Hamoudi, Embolo, Calla.
FC PORTO: Fabiano, Danilo, Maicon, Marcano, Alex Sandro, Herrera, Casemiro, Torres (Neves - 68'), Tello Quintero - 81'), Martinez, Brahimi
Akiba: Helton, Martins Indi, Quaresma, Quintero, Evandro, Ruben Neves, Aboubakar.




«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani