Select Menu
Select Menu

Sports

Sports

Entertainment

Music

Video

News

Video

» » Tundaman,Matonya Wamaliza ‘Bifu Lao


TZ MZUKA 08:15 0


Lile bifu la wasanii wa Bongo Fleva,Tundaman na Matonya lililodumu kwa muda wa miaka nane limemalizwa leo kwenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM. 

Tundaman ndiye aliyekuwa wa kwanza kuingia kwenye kipindi ambapo leo alikuwa akizungumza na mashabiki wake na kuitambulisha ngoma yake mpya iitwayo ‘Achana na Mimi’ ambapo mtangazaji wa kipindi hicho,Husna Abdul alimuuza kuhusiana na bifu na Matonya alisema hana tatizo naye.

Ndipo Husna alipomuuliza kuwa kama akitokea Matonya kwa muda huo anaweza kuongea naye na kupanishwa alisema kuwa hata akitokea ataongea naye ingawa hajaonana naye tangu mwaka 2007.
Msanii Matonya alipigiwa simu na kukutana na Tundaman kwenye kipindi na kupatanishwa bifu lao na kuondoka pamoja kuelekea studio ambayo bado hawajaiweka wazi kufanya ngoma yao ya pamoja.


Wasanii hao kwa vipindi tofautitofauti walikuwa wakituhumiana mambo mbaimbali huku Tundaman alishawahi kulalamika kuwa alimtungia Matonya wimbo wa Vaileth ambao ulifanya vizuri lakini msanii huyo hakuwahi kumshukuru wala kumtaja kwenye ‘interview’.

«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani