FULL TIME: CRYSTAL PALACE 1 vs 2 MANCHESTER UNITED, MAROUANE FELLAINI AIBEBA UNITED , AIPA BAO LA USHINDI UGENINI SELHURST PARK!
TZ MZUKA
02:05
0
2-1 Fellaini akisimamisha mashabiki Uwanjani baada ya kufunga bao la pili![](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_sJdhI4n_NwrkkJx6GrgTJsg0WgqbEMHMwYTAZQ5lw_4tfqDCm-Pq8u4sf4yFGDQdPksyhhna5fAGNPU2j4-T42u7x_Ak0QxLDyT4de8MeqB6uwOmPqSBrv5KuwTj4c8w4zlN1oKTnNwagIKLLnIUGsNGUlreIquSaj7bFDzJdtkh8pD46F6k8s7JLtPb0u=s0-d)
Bao la Dakika ya 78 la Marouane Fellaini limewapa Manchester United ushindi wa Bao 2-1 kwenye Mechi ya Ligi Kuu England waliyocheza Ugenini Selhurst Park na Crystal Palace.
Ushindi huu umewachimbia Man United kwenye Nafasi ya 4 wakiwa Pointi 7 mbele ya Timu ya 5 Liverpool ambayo ndiyo pekee inaweza kuwang'oa Man United kwenye nafasi hiyo na kuwanyima kucheza UEFA msimu ujao.
![](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_syj7GyiH9PElqBvRVejN3TBwX5n6jzEpOeHcXMBcfqX3Fv3olnZ0TPURw5yFF9rrgEVut2D8S8GnmnlgP8H4DeHAlLc2RzxWlXpOQQc1S0YEZF37PWLKUZAXPKjBtcIIKgdcLzVG-lViImq8uEWFWV5_SkOUdgZOJir1_V97D3Qi34DbdhR5yaxEj2GrF8=s0-d)
Man United walitangulia kufunga katika
Kipindi cha Kwanza katika Dakika ya 19 kwa Penati ya Juan Mata ambayo
ilikuja baada ya Krosi ya Ashley Young kushikwa na Scott Dann.
Palace walisawazisha Dakika ya 57 kwa Frikiki ya Jason Puncheon iliyobabatiza mtu na kutinga lakini Krosi ya Ashley Young ilimfikia Fellaini aliefunga kwa Kichwa katika Dakika ya 78 na kuwapa Man United ushindi muhimu.
Ili kuhakikisha wanamaliza ndani ya 4 Bora bila kujali nini Liverpool wanafanya, Man United wanahitaji Pointi 3 tu katika Mechi zao mbili zilizobaki.
Man United wamebakisha Mechi moja Old Trafford na Arsenal na Ugenini na Hull City.
Lakini ikiwa Liverpool Jumapili watafungwa na Chelsea au kutoka Sare, njia ni nyeupe kwa Man United.
Fellaini akifanya yake dakika ya 78, akitupia kwa kichwa na kufanya 2-1
Shabiki aliingia Uwanjani baada ya Fellaini kusawazisha!
Raha ya Ushindi bwaaanae!!!
Chupchupuu!!!
Marouane
Fellaini aliifungia Manchester United bao la pili na kufanya 2-1 dakika
ya 78 na mtanange kumalizika United wakiibuka kidedea kwenye Uwanja wa
Selhurst Park, London mbele ya mashabiki 25009. Ushindi huu wa United
unawapa Matumaini ya Kucheza Klabu Bingwa Ulaya msimu Ujao kwani
wamefanikiwa kupata pointi 68 na wapo ndani nne bora wakiwa pia nafasi
ya nne.
Ashley Young akishangilia!
Jason Puncheon dakika ya 57 kipindi cha pili alisawazisha bao na kufanya 1-1.
Jason Puncheon akishangilia bao lake
1-1
Jason Puncheon baada ya kuweka sare
Juan Mata akichonga penati.
Mpaka nyavuni!
Mata akishangilia
Pongezi kwa Mata
Mchezo
huu pia Umemalizika ukimwachia Majeraha Luke Shaw na kulazimika
kuondolewa Uwanjani na huku Wayne Rooney akipumzishwa baada ya kuumia
Mguu.
Luke Shaw kaumia tena na Hapa ni Dokta akimcheki kwa karibu sana
Luke Shaw kaumia tena na kulazimika kuondolewa Uwanjani
Meneja wa Newcastle United Alan Pardew alipata muda akateta na wachezaji wake na kuwapa mbinu
Luke Shaw akiondolewa Uwanjani huko Ugenini Selhurst Park
Rooney nae yale yale!
Rooney alipumzishwa!
Wachezaji wa Crystal Palace wakimsimamia Mwamuzi Michael Olivier baada ya kutoa penati kwa United
Juan
Mata dakika ya 19 kipindi cha kwanza aliifungia United bao kwa mkwaju
wa penati nao Crystal Palace walisawazisha kupitia mpira wa adhabu frii
kiki iliyofungwa na Jason Puncheon dakika ya 57 kipindi cha pili na
kufanya 1-1.
Bao la Dakika ya 78 la Marouane Fellaini limewapa Manchester United ushindi wa Bao 2-1 kwenye Mechi ya Ligi Kuu England waliyocheza Ugenini Selhurst Park na Crystal Palace.
Ushindi huu umewachimbia Man United kwenye Nafasi ya 4 wakiwa Pointi 7 mbele ya Timu ya 5 Liverpool ambayo ndiyo pekee inaweza kuwang'oa Man United kwenye nafasi hiyo na kuwanyima kucheza UEFA msimu ujao.
Palace walisawazisha Dakika ya 57 kwa Frikiki ya Jason Puncheon iliyobabatiza mtu na kutinga lakini Krosi ya Ashley Young ilimfikia Fellaini aliefunga kwa Kichwa katika Dakika ya 78 na kuwapa Man United ushindi muhimu.
Ili kuhakikisha wanamaliza ndani ya 4 Bora bila kujali nini Liverpool wanafanya, Man United wanahitaji Pointi 3 tu katika Mechi zao mbili zilizobaki.
Man United wamebakisha Mechi moja Old Trafford na Arsenal na Ugenini na Hull City.
Lakini ikiwa Liverpool Jumapili watafungwa na Chelsea au kutoka Sare, njia ni nyeupe kwa Man United.