Select Menu
Select Menu

Sports

Sports

Entertainment

Music

Video

News

Video

» » LIGI KUU ENGLAND: CHELSEA SARE, ARSENAL USHINDI, MAN UNITED YAPIGWA NA SWANSEA!


TZ MZUKA 09:18 0

Penati ya Santi Cazorla na Bao la Olivier Giroud, yote Kipindi cha Kwanza, yamewapa Arsenal wa Ugenini wa Bao 2-1 walipoichapa Crystal Palace na kutwaa Nafasi ya 3 kwa kuishusha Man United Nafasi ya 4.
Bao pekee la Palace lilifungwa Dakika ya 90 na GlennMurray.
VIKOSI:
Crystal Palace: Speroni,Ward, Delaney, Dann, Souare, Mutch, Ledley, Puncheon, Zaha, Gayle, Campbell
Akiba: Hennessey, Hangeland, Kelly, Jedinak, Bolasie, Ameobi, Murray.
Arsenal: Ospina, Chambers, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Coquelin, Cazorla, Welbeck, Ozil, Alexis, Giroud
Akiba: Szczesny, Gibbs, Bellerin, Gabriel, Wilshere, Rosicky, Walcott.
REFA: Mark Clattenburg


Chelsea 1 Burnley 1
Chelsea, wakichezwa kwao Stamford Bridge, wametoka Sare 1-1 na Burnley ambayo inapigana isishushwe Daraja.
Chelsea walitangulia kufunga kwa Bao la Branislav Ivanovic la Dakika ya 14 lakini wakawa pungufu katika Dakika ya 70 pale Nemanja Matic alipopewa Kadi Nyekundu alipolipizia Rafu toka kwa Ashley Barnes.
Burnley walisawazisha kwa Bao la Kichwa la Ben Mee kufuatia Kona ya Dakika ya 81.
VIKOSI:
Chelsea: Courtois; Ivanovic, Zouma, Terry, Filipe Luis; Matic, Fabregas; Cuadrado, Oscar, Hazard; Diego Costa
Akiba: Cech, Azpilicueta, Cahill, Ramires, Willian, Drogba, Remy
Burnley: Heaton; Trippier, Shackell, Keane, Mee; Boyd, Jones, Arfield, Kightly; Barnes, Ings
Akiba: Gilks, Duff, Wallace, Vokes, Reid, Jutkiewicz, Ward.
REFA: Martin Atkinson

Swansea 2 Manchester United 1
Kama walivyofanya katika Mechi ya ufunguzi wa Msimu huu huko Old Trafford Mwezi Agosti, Swansea Leo hii wakiwa kwao Liberty Stadium wameipiga Man United Bao 2-1.
Man United walitangulia kufunga kwa Bao la Anders Herrera la Dakika ya 28 na Swansea kusawazisha Dakika ya 30 kwa Bao la Ki Sung-yueng na kisha Gomis kuwapa ushindi kwa bao la kibahati baada ya Shuti la Mita 25 la Jonjo Shelvey kumbabatiza usoni na kumhadaa Kipa David de Gea.
VIKOSI:
Swansea: Fabianski; Naughton, Fernandez, Williams, Taylor; Cork, Shelvey, Ki, Sigurdsson, Routledge; Gomis
Akiba: Tremmel, Rangel, Amat, Britton, Montero, Emnes, Oliveira.
Manchester United: De Gea; McNair, Jones, Rojo, Shaw; Blind, Fellaini, Herrera, Di Maria; Rooney, Van Persie
Akiba: Valdes, Smalling, Januzaj, Mata, Valencia, Young, Falcao.
REFA: Neil Swarbrick


 MATOKEO KAMILI:
Aston Villa 1 Stoke 2     
Chelsea 1 Burnley 1       
Crystal Palace 1 Arsenal 2
Hull 2 QPR 1
Sunderland 0 West Brom 0      
Swansea 2 Man United 1
2030 Man City v Newcastle

Credit To;: www.sokaintanzania.com

«
Next
Chapisho Jipya
»
Previous
Taarifa za zamani