PICHAZ;Alikiba na Jokate wathibitisha uhusiano wao hebu zicheki picha zao walizoziweka instagram
TZ MZUKA
03:52
0
Na sasa penzi la Jokate Mwegelo na Alikiba limefikia hatua ambayo haliwezi kuwa siri tena. Wawili hao wamekuwa wakidaiwa kuwa wapenzi kwa miezi kadhaa sasa lakini bado binafsi hawajeza kukubali wala kukataa.
Lakini sasa huenda hatua za awali za kuelekea kuuweka hadharani uhusiano huo zimeanza kufanyika. Alianza Jokate aliyepost selfie kwenye Instagram akiwa na msanii huyo aliyejipa jina la King Kiba na kutoandika chochote. Picha hiyo imepata likes 13,215 na comments 824.
Naye Kiba jana alipost selfie nyingi kwenye akaunti yake ya Instagram na kuandika: Pop It In @jokatemwegelo #KingKiba.” Picha hiyo imevutia likes 8108 na comments 680.